Thursday, February 16, 2017

MAGEREZA WAZINDUA MAZOEZI YA VIUNGO JIJINI DAR

Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (mwenye kofia) akiongoza watumishi  wa Makao Makuu ya  Jeshi la Magereza katika uzinduzi wa mazoezi ya viungo, uzinduzi huo ulifanyika katika ufukwe wa Bahari ya Hindi. Wa tatu kulia Naibu Kamishna wa Magereza (DCP) Edith Mallya
Baadhi ya maafisa, askari na watumishi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza wakiongozwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Dkt. Juma Malewa (wa tatu kushoto) pamoja na Naibu Kamishna  wa Magereza (DCP) Edith Mallya (wa nne kulia) katika kufanya mazoezi ya viungo ufukweni mwa Bahari ya Hindi 
Sehemu ya maafisa, askari na watumishi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika mazoezi ya viungo katika ufukwe wa Bahari ya Hindi ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa ufanyaji wa mazoezi ya viungo kwa watumishi wa Jeshi hilo, mazoezi ya viungo hufanyika mara mbili kwa wiki siku ya Jumatano na Ijumaa kuanzia saa 10 jioni.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga  (wa pili kushoto) akiwa pamoja na watumishi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika uzinduzi wa mazoezi ya viungo katika ufukwe wa Bahari ya Hindi jijini Dar es salaam. 
Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (mwenye kofia) akiongoza uzinduzi wa zoezi la ufanyaji wa mazoezi ya viungo kwa maafisa, askari na watumishi raia katika ufukwe wa Bahari ya Hindi mwishoni mwa juma.
Baadhi ya watumishi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika mazoezi ya kunyoosha viungo siku ya uzinduzi wa zoezi la ufanyaji mazoezi ya viungo kwa Jeshi hilo.

Sehemu ya watumishi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza katika mazoezi ya kunyoosha viungo siku ya uzinduzi wa zoezi la ufanyaji mazoezi ya viungo yalizinduliwa mwishoni mwa juma katika ufukwe wa Bahari ya Hindi mwishoni mwa juma.

(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Makao Makuu ya Magereza).