Friday, March 17, 2017

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA MAGEREZA, JIJINI DAR

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb) akiwasili leo Machi 17, 2017 katika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam tayari kwa ufunguzi  wa Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza(wa kwanza kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akisaini katika kitabu cha wageni kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kushoto) akiwa meza kuu na  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(wa pili kulia) kabla ya ufunguzi wa Mkutano huo. Wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga (wa kwanza kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba kufungua rasmi Mkutano huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akiwasilisha hotuba yake kwenye Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini hotuba fupi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba (hayupo pichani).
Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Simon Mwanguku akiwasilisha mada katika Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza. Mkutano huo umefanyika leo Machi 17, 2017 katika Bwalo Kuu la Maafisa Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha Brass Band ya Jeshi la Magereza kikitumbuiza kwenye ufunguzi wa huo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Jeshi la Magereza Wastaafu(waliosimama mstari wa nyuma).Wa pili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa, wa kwanza kushoto ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga na wa kwanza kulia ni Naibu Kamishna wa Magereza, Edith Mallya mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza 

(Picha zote na ASP  Deodatus Kazinja).