Tuesday, April 11, 2017

MAHAFALI YA PILI KIDATO CHA SITA BWAWANI SEKONDARI YAFANA MKOANI PWANI

Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Bwawani, Gaston Sanga akivishwa skafu na mmoja ya wa wanafunzi wa kikundi cha skauti cha shule hiyo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mahafali ya pili ya Kidato cha sita shuleni hapo leo Aprili 11, 2017.
Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Bwawani, Gaston Sanga akikagua kikundi cha skauti cha shule hiyo kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Bwawani, Gaston Sanga akisalimiana na baadhi ya wazazi na wajumbe wa Bodi ya shule hiyo.
Muonekano wa madarasa mapya yaliyojengwa tayari kwa matumizi katika Shule ya Sekondari Bwawani, Mkoani Pwani.
Muonekano wa ndani wa Bweni la Wasichana lililokamilishwa kujengwa tayari kwa matumizi katika Shule ya Sekondari Bwawani, Mkoani Pwani
Maandamano ya wahitimu, wazazi na wageni waalikwa yakiongozwa na kikundi cha Brass Bendi kuelekea katika viwanja vya mahafali ya Kidato ya sita katika Shule ya Sekondari Bwawani, Mkoani Pwani.
Mkuu wa Shule ya Shule ya Sekondari Bwawani, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Emmanuel Lwinga akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika mahafali hayo.
Mgeni rasmi Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Gaston Sanga akitoa hotuba fupi kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Wahitimu wa Kidato cha Sita wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza aliyewakilishwa na Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala Gaston Sanga.
Mmoja wa wahitimu wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Bwawani iliyopo Mkoani Pwani akipokea cheti cha kuhitimu elimu hiyo.
Baadhi ya Wanafunzi wa Bwawani Sekondari wakionesha ubunifu wa mavazi mbalimbali katika mahafali ya pili ya kidato cha Sita shuleni hapo.
Mgeni rasmi Kamishna wa Magereza Divisheni ya Fedha na Utawala, Gaston Sanga(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Kidato cha Sita(waliosimama) katika Mahafali ya pili ya Shule ya Sekondari Bwawani(wa pili kushoto) ni Kamishna Mkuu wa Magereza Mstaafu Jumanne Mangala, (wa tatu kulia) ni Naibu Kamishna wa Magereza Edith Malya na wa pili kulia ni Mkuu wa Chuo cha Urekebishaji Ukonga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Gideon Nkana

(Picha zote na Jeshi la Magereza).