Thursday, November 6, 2014

Mkutano wa wadau wa kupokea maoni juu ya sera ya Taifa ya Magereza wamalizika Wilayani Bagamoyo

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw.  Mbarak Abdulawakil akitoa hotuba ya Ufungaji wa Mkutano wa Wadau uliohusu upokeaji wa maoni ya Sera ya Taifa ya Magereza. Mkutano huo wa siku mbili umefanyikia katika Hoteli ya Livingstone Bagamoyo ambapo wadau wamepitia rasimu hiyo na kutoa maoni kikamilifu Novemba 05, 2014.
Wadau wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufungaji wa Mkutano wa Wadau uliohusu upokeaji wa maoni ya Sera ya Taifa ya Magereza Novemba 05, 2014 katika Hoteli ya Livingstone Bagamoyo .
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw.  Mbarak Abdulawakil kutoa hotuba ya Ufungaji wa Mkutano wa Wadau uliohusu upokeaji wa maoni ya Sera ya Taifa ya Magereza.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(katikati) akipitia makabrasha wakati wa majadiliano ya rasimu ya Sera ya Taifa ya Magereza(kulia) ni Mkurugenzi Idara ya Malalamiko Wizara ya Mambo ya Ndani, Bw. A. Shio(kushoto) ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw.  Mbarak Abdulawaki. 
Mchumi kutoka Wizara ya Fedha, Bi. Deonesia Mjema akichangia maoni katika rasimu ya Sera ya Taifa ya Magereza kabla ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw.  Mbarak Abdulawakil kutoa hotuba ya Ufungaji wa Mkutano wa Wadau uliohusu upokeaji wa maoni ya Sera ya Taifa ya Magereza.
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma malewa akitolea ufafanuzi wa Haki za Wafungwa wanazostahili kupatiwa wawapo Magerezani wakati wa majadiliano Sera ya Taifa ya Magereza Novemba 05, 2014 katika Hoteli ya Livingstone Bagamoyo(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).