Monday, December 29, 2014

Maafisa, Askari na Watumishi wa Jeshi la Magereza wapatiwa mafunzo ya jinsia, Rombo Green View Hotel-Jijini Dar es Salaam

Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba fupi kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Jinsia kwa Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza, leo Desemba 29, 2014 katika Ukumbi wa Rombo Green View Hotel. Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku mbili ambapo yatafungwa rasmi kesho Desemba 30, 2014(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunura(wa pili kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Augustino Mboje(kulia) ni Mkuu wa Mafunzo ya Kijeshi wa Magereza, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Mbarak Semwenza.
Baadhi ya Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza wanaoshiriki Mafunzo ya Jinsia katika Ukumbi wa Rombo Green View Hotel wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi. Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku mbili ambapo yatafungwa rasmi kesho Desemba 30, 2014.
Mshiriki wa Mafunzo ya Jinsia kutoka Makao Makuu ya Magereza, Mkaguzi wa Magereza, Amina Lidenge akijitambulisha kabla ya Ufunguzi rasmi wa Mafunzo ya Jinsia.
Mtoa Mada wa Kwanza kutoka Wizara ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bi. Magreth Mussai akiwasilisha Mada yake kuhusiana na dhana ya Jinsia kama anavyoonekana katika picha.
Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa, Askari na Watumishi raia wa Jeshi la Magereza(waliosimama) mara baada ya Ufunguzi rasmi wa Mafunzo ya Jinsia leo Desemba 29, 2014 katika Ukumbi wa Rombo Green View Hotel, (kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunura, (wa pili kushoto) ni Mtoa Mada wa Kwanza kutoka Wizara ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bi. Magreth Mussai(wa pili kulia) ni Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwila, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Luhembe, (kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Augustino Mboje
 
(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).