Thursday, December 4, 2014

Kuitwa kwenye usaili



04 Desemba 2014

KUITWA KWENYE USAILI

Jeshi la Magereza linawatangazia wafuatao kufika kwenye usaili kwa nafasi walizoomba. Usaili huo utafanyika kuanzia tarehe 10/12/2014 mpaka tarehe 17/12/2014 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Magereza Ukonga Jijini Dar es salaam kuanzia 2:00 asubuhi kwa mujibu wa tarehe za makundi kama yalivyoainishwa. Kwa wale wa kidato cha Nne na Sita waliosailiwa kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wasubiri maelekezo mengineyo. Aidha wale ambao hawakuona majina yao hapa wahesabu kuwa hawakufanikiwa.

Waombaji wanatakiwa kuzingatia  yafuatavyo;-

i.    Kuja na Vyeti halisi (Original Certificates) vya elimu na ujuzi

ii.    Kuja naCheti halisi cha kuzaliwa,

iii.    Hati za matokeo ya mitihani (Result Slip/Statements) hazitakubaliwa isipokuwa kwa wahitimu ambao vyeti vyao halisi havijatolewa na vyuo husika wakiwa na barua Maalum ya kuthibitisha kwamba vyeti halisi havijatolewa,

iv.    Wahusika watajitegemea kwa nauli za kuja na kurudi, chakula na malazi kwa kipindi chote cha usaili

Tangazo hili pia linapatikana kwenye Mbao za Matangazo zilizopo Bwalo Kuu la Magereza, tovuti ya magereza kwa anwani ya www.magereza.go.tz, gazeti la Uhuru la tarehe 05 Desemba 2014 sanjari na blog ya magereza kwa anwani ya www.magereza.blogspot.com

Imetolewa na Kamishna Jenerali wa Magereza

J.C.Minja

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA


Bofya HAPA kupata orodha ya wanaotakiwa kufika kwenye usaili