Wednesday, March 4, 2015

Maandalizi ya kupanda mlima kilimanjaro-Maafisa na askari wa Jeshi la Magereza

Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya kukimbia katika viunga vya manispaa ya Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro March 6, 2015. Maafisa hao wameweka kambi katika eneo la Gereza Karanga-Moshi.
Sehemu ya  Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali  katika mitaa ya mji wa Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6,2015. Katikati (mwenye vazi jeupe) ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy kutoka Makao Makuu ya Magereza, wa kwanza kulia ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza Mbezi Ramadhani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga na wa kwanza kushoto ni Mkaguzi wa Magereza Jamhuri Yassin kutoka Makao Makuu ya Magereza, Dar es salaam.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya kutembea  katika viunga vya Manispaa ya Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro mnamo Machi 6, 2015. Kutoka kushoto ni Mkaguzi wa Magereza Vicent Magessa kutoka Gereza Bagamoyo Mkoa wa Pwani, Mkaguzi wa Magereza Tumaini Kihampa na Mkaguzi wa Magereza Jamhuri Yassin wote kutoka Makao Makuu ya Magereza.
Maafisa na Askari na baadhi wa watumishi raia wa  Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali ya kupita katika njia ngumu ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6, 2015. Wa sita kutoka mbele ni Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Magereza Estomiah Hamis na wa mwisho ni Mkaguzi wa Magereza Abas Mikidadi
Maafisa na Askari na baadhi wa watumishi raia wa  Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali ya kupita katika njia ngumu ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6, 2015.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya viungo  baada ya kutembea na kukimbia katika viunga vya Manispaa ya Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro mnamo Machi 6, 2015.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakipata kifungua kinywa baada ya mazoezi mazito ya maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6,2015. Maafisa hao wako kambini eneo la Gereza Karanga mjini Moshi.
Baadhi wa washiriki wa Kilimanjaro Marathon Machi 1, 2015 mbio ambazo baadhi ya  Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza walishiriki ikiwa ni maandalizi ya kupanda Mlima Kilimanjaro mnao Machi 6, 2015. 

Picha zote na Mkaguzi wa Magereza Deodatus Kazinja