Saturday, March 14, 2015

Mafunzo ya awali ya askari wa magereza kozi na. 27 yaendelea vyema chuo Kiwira, Mbeya

Askari Wanafunzi(Recruits) wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza Kozi Na. 27 wakiendelea na masomo kwa vitendo katika Gwaride la silaha kama wanavyoonekana kikakamavu wakiwa na Walimu wao uwanjani huku silaha zao zikiwa begani.
Askari Wanafunzi wa Mafunzo ya Uaskari Magereza Kozi Na. 27 wakiendelea na somo la Gwaride la Salaam ya Utii wakiwa na silaha kama inavyoonekana katika picha.
Bango Kuu linaloonyesha unapoingia Chuo cha Mafunzo ya Uaskari Magereza kilichopo Kiwira, Mkoani Mbeya.
Askari Wanafunzi wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakiendelea na masomo ya Darasani. Katika Mafunzo hayo hujifunza masomo mbalimbali ikiwemo Utawala na Uendeshaji wa Magereza, Sheria zinazoongoza Jeshi la Magereza, Ustawi wa Jamii, Afya, Uraia na Utawala na Uongozi

(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).