Saturday, January 7, 2017

KAIMU KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT JUMA MALEWA AFANYA MABADILIKO YA UONGOZI KWA MAAFISA WAANDAMIZI WA MAGEREZA

Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Ally Malewa(pichani) amefanya Mabadiliko ya Uongozi kwa baadhi ya Wakuu wa Magereza Mikoa na vituo mbalimbali hapa nchini.

Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Katos Rugainunura amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza sehemu ya Utawala na nafasi yake inakaimiwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Mzee Nyamka aliyekuwa Mkuu wa Utawala Magereza Mkoani Morogoro. Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Antonino Kilumbi  aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma amehamishwa kwenda Makao Makuu ya Magereza kuwa Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Julius Sang’udi aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya.

Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Anderson Kamtiaro anaenda kuwa Afisa Mnadhimu Magereza Mkoani Arusha na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Hassan Mkwiche ambaye alikuwa ni Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa Gereza Same Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Evarist Katego anakwenda kuwa Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Uwesu Ngarama amehamishiwa Makao Makuu kuwa Boharia Mkuu wa Jeshi na nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Afisa Mipango wa Jeshi ACP Athuman Kitiku.  

Aidha,  aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoani Mtwara,  Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Musa Kaswaka anakwenda Makao Makuu Kitengo cha Ukaguzi  na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Ismail Mlawa aliyekuwa Mkuu wa Kiwanda cha Samani Gereza Kuu Ukonga. Aliyekuwa Afisa Mdhibiti wa Fedha wa Jeshi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Gideon Nkana anakwenda kuwa Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga, Dar es Salaam na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Chacha Jakson.

Wengine ni pamoja na aliyekuwa Afisa Mnadhimu wa Magereza Mkoa wa Mbeya ACP Kijida Mwakingi anakaimu nafasi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Abdalah Misanga anayetoka Gereza Mgumu kwenda kuwa Mkuu wa Gereza Msalato, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP  John Itambu anayetoka Gereza Kilosa kwenda kuwa Mkuu wa Kiwanda cha Samani Gereza Kuu Ukonga.

Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Erasmus Kundy anayetoka Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga kwenda Makao Makuu Kitengo cha Habari, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Julius Ntambala aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Ujenzi Makao Makuu anabakia Makao Makuu Kitengo cha ujenzi kuwa Msaidizi wa Mkuu wa Kitengo, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Sylivester Mrema  anayetoka Gereza Idete kwenda Gereza Ubena kuwa Mkuu wa Gereza.

Aliyekuwa Mkuu wa Gereza Ubena Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Shaba Zephania anakwenda Magereza Mkoa wa Pwani kuwa Afisa Mnadhimu, Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Solomon Urio anayetoka Makao Makuu kwenda Magereza Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Afisa Mnadhimu pamoja na aliyekuwa Boharia Mkuu wa Jeshi la Magereza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP George Kiria amehamishiwa Makao Makuu Kitengo cha Uhasibu .

Mabadiliko hayo ni ya kawaida na yanalenga kuboresha utendaji kazi na ufanisi wa Jeshi la Magereza.

Imetolewa na:

Lucas Mboje - ASP
Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza
Makao Makuu ya Magereza Tanzania Bara
07 Januari, 2017.