Banner

Banner

Tuesday, March 18, 2025

KAMATI YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAFANYA UKAGUZI ZAHANATI YA GEREZA SINGIDA.

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya Ukimwi, ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Hassan Mtenga, imefanya ziara ya ukaguzi katika  Zahanati ya Gereza Singida, leo machi 17, 2025, ikiwa na lengo la kutathmini huduma zinazotolewa zahanati hapo.

 

Katika ukaguzi huo  Kamati ilikagua huduma za CTC, chumba  cha Maabara, chumba cha daktari, chumba cha takwimu pamoja na chumba cha  dawa,  pia  waliweza kufanya  kikao na Kamati ya mkoa ya Afya  na masuala  ya  Lishe  na kuupongeza uongozi wa  jeshi la magereza kwa huduma  wanazotoa katika zahanati hiyo.


"Hongereni kwa kazi kubwa na nzuri ambayo  mnafanya, tumejionea ,  DMO pamoja na  dactari mkuu wa mkoa  tunaomba  mtatue changamoto ndogondogo zinazokabili  zahanati ya gereza" alisema  Mhe. Mtenga


Aidha Mhe. Mtenga ametoa rai kwa Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na wabunge wote nchini  kujenga utamaduni wa kutembelea  Magereza mbalimbali ili kubaini changamoto zinazoyakabili na kuzitafutia ufumbuzi.


Kwaupande wake Kamishina Jenerali wa  Magereza  Jeremia  Yoram Katungu  ameishukuru  Kamati ya Bunge  ya Afya na Masuala ya  Ukimwi kwa kutembelea na kukagua Zahanati hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote waliyoyatoa ili kuboresha huduma za Afya