Wakufunzi na wanafunzi kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC),leo Machi 12,2025 wamefanya ziara Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Msalato jijini Dodoma, lengo likiwa ni kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza.
Akiongea katika hotuba yake Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza (CGP)Jeremiah Yoram Katungu amekipongeza Chuo hicho kwa kufanya ziara Makao Makuu ya Jeshi la Magereza huku akisema uhusiano huo unalenga kujenga na kuimarisha katika muktadha wa kulinda mataifa yetu kuendelea.
Kwa upande wake Brigedia Jenerali C.J.Ndiege ambaye ni mkuu wa msafara kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) amesema kuwa miongoni mwa malengo ya Chuo hicho ni kutoa mafunzo ya kimkakati katika masuala ya ulinzi kwa sekta binafsi, kikanda na kimataifa.
Aidha katika ziara hiyo kulitolewa wasilisho la matumizi ya teknologia ya habari magerezani,ambapo wasilisho hilo lilitolewa na Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Kizito Jaka.
Pamoja na mambo mengine washikiri katika ziara hiyo walipata fursa ya kupanda miti eneo linalozunguka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza.