Thursday, June 4, 2015

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi awaongoza waombolezaji kuuaga mwili wa marehemu kamishna mkuu mstaafu wa jeshi la Magereza, Onel Malisa jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe akitoa heshima za mwisho kwa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa ambaye ameagwa leo Kijeshi Juni 04, 2015 katika Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga Jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwa mazishi kwao Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Mwili wa Marehemu, Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa ukiwa umebebwa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza tayari kwa zoezi la kuagwa Kijeshi katika Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akiwa amesimama wakati mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa ulipokuwa ukiwasili katika Viwanja vya Chuo Cha Maafisa Magereza Ukonga(katikati) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe(kulia) ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akisaini katika Kitabu cha Maombolezo kabla ya kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu wa Magereza Mstaafu Onel Malisa.

Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini salaam mbalimbali za rambirambi zilizokuwa zikitolewa katika hafla ya kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu, Onel Malisa.
 
Kiongozi Mwakilishi wa Wastaafu wa Jeshi la Magereza, Naibu Kamishna Mstaafu wa Magereza, John Nyoka akitoa salaam za rambirambi.
Gadi Maalum ya Maafisa wa Jeshi la Magereza kwa ajili ya paredi la kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Jeshi la Magereza, Onel Malisa.
 
Umati wa ndugu na Jamaa waliojitokeza kuuaga mwili wa Marehemu Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Onel Malisa.